Makala Mpya

Kitendo cha kula Moyo Syria chalaaniwa

Kitendo cha kula Moyo Syria chalaaniwa

 Kanda ya video ambayo inaonekana kuonyesha muasi mmoja nchini Syria akila Moyo wa mwanajeshi aliyefariki, imelaaniwa vikali. Shirika la Marekani la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch, limemtaja muasi huyo kama Abu Sakkar, muasi anayejulikana sana kutoka mji wa Homs, na kusema kuwa vitendo vyake ni vya uhalifu wa kivita. Chama rasmi cha upinzani

Hali ya hatari yatangazwa katika majimbo 3 Nigeria

Hali ya hatari yatangazwa katika majimbo 3 Nigeria

Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria ametangaza hali ya hatari katika majimbo matatu ya nchi hiyo kufuatia kushtadi visa vya uhalifu na hujuma vinavyotekelezwa na wanamgambo wa Boko Haram  kwenye majimbo hayo. Rais Jonathan amesema majimbo yatakayoathiriwa na uamuzi huo ni pamoja na Borno, Yobe na Adamawa. Kiongozi huyo amesema hali mbaya ya usalama imeilazimisha serikali

Wanne wafariki baada ya jengo kuporomoka Rwanda

Wanne wafariki baada ya jengo kuporomoka Rwanda

Habari kutoka Rwanda zinasema watu wasiopungua wanne wamepoteza maisha baada ya jumba la ghorofa 4 kuporomoka katika mji wa Nyagatare, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Habari zaidi zinasema zaidi ya watu 100 wamefukiwa kwenye vifusi. Wizara ya kukabiliana na majanga imesema juhudi zinafanywa ili kuwaokoa wale waliofukiwa. Jumba lililoporomoka lilikuwa likiendelea kujengwa na baadhi ya

Boti yazama Myanmar; Waislamu 10 wahofiwa kufa

Boti yazama Myanmar; Waislamu 10 wahofiwa kufa

  Habari kutoka Myanmar zinasema kuwa boti iliyokuwa imewabeba Waislamu wa kabila la Rohingya imezama na kusababisha vifo vya takribani watu 10. Habari zaidi zinasema boti hiyo ilikuwa imebeba watu kupita kiasi na hadi sasa zaidi ya watu 50 hawajulikani waliko. Wengi wa wasafiri walikuwa akina mama na watoto ambao walikuwa wakikimbia mvua kubwa zinazoendelea

Mauaji ya wanaharakati wa Uturuki; uchunguzi waanza

Mauaji ya wanaharakati wa Uturuki; uchunguzi waanza

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC amesema kuwa, ofisi yake imeanza kuchunguza shambulizi la makomandoo wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya meli ya misaada ya Uturuki iliyokuwa ikielekea Ukanda wa Gaza mwaka 2010. Fatou Bensouda amesema uchunguzi huo unalenga kubaini iwapo jinai za kivita au dhidi ya binadamu zilitendeka.

Russia yamtimua mwanadiplomasia jasusi wa US

Russia yamtimua mwanadiplomasia jasusi wa US

Serikali ya Russia imemfukuza mwanadiplomasia wa ngazi za juu katika ubalozi wa Marekani mjini Moscow baada ya kubainika kuwa anashirikiana na shirika la kijasusi la CIA. Maafisa wa usalama wa Russia wamemkamata Ryan Fogle alipojaribu kumlipa afisa wa usalama ili amfanyie ujasusi. Televisheni ya Russia imemuonyesha jasusi huyo wa Marekani akiwa amefungwa pingu. Vifaa mbalimbali

Nahjul Balagha

Nahjul Balagha

Stay tuned to IBNTV tonight  at 10.oopm and watch a  brand new episode of  ‘The Wide Angle.Sheikh Abbas Alawi and Sister Zishaan Karim discuss Nahjul Balagha. Log in to this website daily and get updated as to when this episode will be aired online

REFLECTIONS ISSUE 23

REFLECTIONS ISSUE 23

Allah sets forth an example: A man jointly owned by several contending masters, and a man belonging entirely to one man: are the two equal in comparison? All praise belongs to Allah; but most of them do not know. – Sura Zumar, 39:29 The Holy Quran abounds with parables, or examples. It is part of

Mkutano wa kuichangia Mali kufanyika Ubelgiji

Mkutano wa kuichangia Mali kufanyika Ubelgiji

Mkutano wa kimataifa utaanza  kesho huko Brussels, mji mkuu wa Ubelgiji kwa lengo la kukusanya kiasi cha  euro bilioni moja na milioni mia tisa za kuisaidia nchi ya Mali. Laurent Fabius Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ufaransa amesema kuwa, wawakilishi kutoka karibu nchi 100 wakiwemo wakuu wa nchi 10 watahudhuria kwenye mkutano

UNAMID yataka waasi waache machafuko Sudan

UNAMID yataka waasi waache machafuko Sudan

Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa UNAMID huko Darfur Sudan vimeyataka makundi ya waasi kusitisha machafuko na vitendo vya utumiaji mabavu. Taarifa ya UNAMID imezitaka pande zote zinazozona katika jimbo la Darfur hususan makundi yanayobeba silaha na ambayo hayajajiunga na hati ya makubaliano ya amani kusitisha vitendo vya hujuma