Mafunzo ya semina ya vyombo vya habari-Desemba 12 2009
Hii ilikuwa semina ya kwanza we washiriki wa Al-Itrah Foundation na kushirikiana na waratibu ambao ni Nyota Foundation. Timu ya wanahabari huvutika kuona uwezekano wa rasilimali watu wakitumia vipawa vyao katika suala zima la kuandaa habari kwa manufaa ya umma.
Waratibu wanayomatumaini na matarajio kwamba mambo haya yatakuwa yakiendelea kwa muda mrefu katika kuwaelimisha washiriki ikiwa ni pamoja na kuwapatia zana husika kwa ajili ya maendeleo ya mbeleni.
Jumla kulikuwa na idadi ya washiriki 47 ikiwa ni pamoja na wanawake. semina hii ilidumu kwa karibu masaa 8 ikiendeshwa na al-Bayaan Media Group Company-DSM.
Masomo yaliyowasilishwa kwa wanasemina wakati wa warsha ni haya yafuatayo:
VIANZIO VYA KUANDAA KIPINDI
UTAYARISHAJI BORA WA KIPINDI.
MAHOJIANO
UWANDISHI WA SCRIPT
UTANGAZAJI BORA WA KIPINDI
UWANDAAJI mzuri WA RATIBA YA KIPINDI
Washiriki walikuwa na msisimko sana na warsha hiyo na kwamba wameomba kuendelea na mafunzo ya ndani kwa ajili ya Redio Maarifa na Runinga ya Ibn.





Tweet This
Share on Facebook
Digg This
Save to delicious
Stumble it
RSS Feed



